More Highlights...
- Amb. Herbert Mrango - Deputy Permanent Secretary…
- Ministry of Infrastructure - Budget 2010/2011
- Ziara ya Katibu Mkuu Omari Chambo kutembelea mradi…
- UTEUZI WA MWENYEKITI WA BODI YA CHUO CHA BAHARI…
- BODI MPYA YA TPA
- Floods shut Dar – Dodoma, part of the central…
- Ministry of Infrastructure Development restructured…
- TAARIFA KUHUSU MASUALA YA TRL
- Tanzanian minister highlights China’s contribution…
- EAC Roads Sector Projects
- Ujenzi wa MiundoMbinu na msukosuko wa fedha duniani…
- Kilimanjaro International Airport - KIA
- Daraja la Umoja Kukamilika 2009
- ATCL gets lease to fly again
- Tanzania to use $946m to improve its regional…
Site Search
Reports & Policies
To facilitate provision of an economic, safe and reliable constriction industry, transport and services, meteorology, government buildings...

Ministry of Infrastructure Development
Its mission is to facilitate provision of an economic, safe and reliable construction industry, transport and services, meteorology, electrical and mechanical services, government buildings and stores that meet the needs of the public through development and implementation of appropriate sector policies, strategies and standards.
News and HighlightsUjenzi wa MiundoMbinu na msukosuko wa fedha duniani ukifuatiliwa na mkutano wa wakuu wa AU
Mkutano wa 12 wa wakuu wa Umoja wa Afrika ulifunguliwa tarehe 1 mwezi Februari huko Adis Ababa, makao makuu ya Umoja wa Afrika. Mkutano huo utafanyika hadi tarehe 3, na kauli mbiu ya mkutano huo ni "ujenzi wa miundo mbinu barani Afrika". Viongozi, mawaziri wakuu na wajumbe kutoka nchi zaidi ya 50 wanachama wa umoja huo watajadili ujenzi wa miundo mbinu ya mawasiliano barabarani, nishati barani Afrika, na msukosuko wa fedha duanini. Miundo mbinu barani Afrika bado iko nyuma, hali hii siku zote inazuia maendeleo ya uchumi na jamii barani humo. Hivi sasa Afrika inakabiliwa na changamoto za kuboresha miundo mbinu. Wataalamu waliona kuwa miundo mbinu iliyoko nyuma kila mwaka inapunguza ongezeko la uchumi wa Afrika kwa zaidi ya asilimia moja. Naibu katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa ambaye pia ni katibu mtendaji wa kamati ya uchumi wa Afrika ya Umoja wa Mataifa Bw. Abdoulie Janneh tarehe 29 mwezi Januari kwenye ufunguzi wa mkutano wa 14 wa mawaziri wa mambo ya nje wa bodi ya wakurugenzi ya Umoja wa Afrika alisema, miundo mbinu yenye ufanisi na ya kutegemeka katika mawasiliano ya barabara na nishati ni muhimu sana kwa kutimiza utandawazi wa jamii na uchumi barani Afrika. Sasa barani Afrika watu wanaoweza kutumia umeme wachukua asilimia 40 tu, na baadhi ya nchi za Afrika zilikumbwa na hali ya upungufu na ukosefu wa umeme, hali hii imeathiri vibaya maendeleo ya uchumi. Licha ya hayo, hali iliyoko nyuma ya mawasiliano pia inakwamisha maendeleo ya uchumi. Kutokana na kuwa hali ya siasa barani Afrika inaelekea kwa utulivu, nchi nyingi za Afrika ziliweka mkazo kwanza katika kustawisha uchumi katika ujenzi wa miundo mbinu. Takwimu zilizotolewa na Benki ya dunia zimeonesha kuwa, katika miaka kumi ijayo, ujenzi wa miundo mbinu barani Afrika utahitaji dola za kimarekani bilioni 250, na sekta za mawasiliano na uchukuzi, umeme, maji, na upashanaji wa habari ni sekta muhimu zinazowekezwa na serikali za nchi mbalimbali barani Afrika. Ili kuvuta kampuni za nchi za nje kushiriki kwenye ujenzi wa miundo mbinu, serikali za nchi mbalimbali za Afrika zinatekeleza sera zenye unafuu katika kodi na kutoa ruzuku za mitaji. Waziri wa mambo ya nje wa China Bw. Yang Jiechi alipofanya ziara katika nchi nne ikiwemo Uganda alisema, kauli mbiu ya mkutano huo wa wakuu wa Umoja wa Afrika inaonesha kuwa nchi za Afrika zinatilia maanani kuboresha ujenzi wa miundo mbinu. China inapenda kuimarisha zaidi ushirikiano kati yake na Afrika katika sekta ya miundo mbinu, na inapenda kuendelea kuchangia maendeleo ya jamii na uchumi barani Afrika. Kauli mbiu nyingine ya mkutano huo ni suala la msukosuko wa fedha duniani. Kutokana na kuenea kwa msukosuko huo, athari mbaya iliyosababishwa na msukosuko huo kwa nchi za Afrika ilionekana hatua kwa hatua, na maendeleo endelevu ya Afrika yaliathiriwa vibaya. Msukosuko wa fedha pia utaathiri vibaya juhudi za nchi za Afrika za kupunguza umaskini. Kabla ya hapo viongozi wa China waliitaka jumuiya ya kimataifa ifuatilie hali ya nchi za Afrika, na kutopunguza msaada maendeleo ya Afrika kutokana na msukosuko wa fedha duniani. China pia ilisisitiza kuwa haitapunguza misaada kwa Afrika, na inapenda kudumisha ushirikiano na nchi za Afrika katika suala la mageuzi ya mfumo wa fedha wa kimataifa. |
Reports and Publications
- Ministry of Infrastructure - Budget 2010/2011
- Ziara wa Waziri mikoa ya Morogoro na Ruvuma Machi, 2010
- Ziara ya Waziri wa Miundombinu JNIA, Februari 2010
- First Business Roundtable Meeting Transport Infrastructure Constrains: Challenges and Opportunities
- Creating Sustainable Fiscal Space for Infrastructure: The Case of Tanzania
- Ministry of Infrastructure - Budget 2008/2009
